Wednesday, August 7, 2013

Mtoto wa kiafrika..........


Habari wapendwa, 
Leo nimeguswa kuongelea mtoto wa kiafrika kwa sababu nimeshawahi kuwa mtoto wa kiafrika na kwasasa nina watoto ambao ni waafrika. Nimekuta najiuliza hivi watoto wetu ambao tunawazaa sisi wenye damu ya kiafrika kweli tunawalea kiafrika? Niweza kuwa na ujasiri wa kuongelea watoto wa kiafrika kwasababu mimi ni mwafrika, ila watoto wa kizungu ninawajua kupitia kusoma vitabu vilivyo andikwa na hao wazungu na kupitia sinema ambazo unakuta zinaelezea habari iliyowahi kutokea kweli katika maisha yao ( based on true story)
Sasa basi mtoto ni toka akiwa ndani ya tumbo la mama yake mpaka anapotimiza umri wa miaka 18 hii ni kwatafsiri ya katiba ila kwa sisi wamama ambao tunawatoto mtoto ni toka akiwa ndani ya tumbo la mama yake mpaka kiama atabaki kuwa mtoto.
 

Mama wa kiafrika tuwalee watoto wetu katika maadili na tamaduni za kiafrika ambazo ni zuri na zenye tija, hapa naanza na vyakula: tule vyakula vyetu vya kiasilia kwani nivyakula vyenye lishe na uboro wa juu ukilinganisha na vya wenzetu wazungu. ( tule matunda, mboga, nafaka, na vinywaji ambayo hayajawekewa machemiko kwa ajili ya kuhifaziwa au kutengenezwa). Na watoto wanyonye maziwa ya mama kwa muda mrefu ikiwezekana mpaka hata wakiwa na umri wa miaka miwili.

 
Malezi: malezi ya watoto wa kiafrika yanabidi kuwa yanafuata mila, desturi na tamaduni za kiafrika ambazo ni nzuri ( hapa namaanisha nizile ambazo hazitawafanya watoto kujuta kuwa wa afrika).

Nimengi yakuongea kwenye swala la mtoto wa Kiafrika, tutakuwa tunaongelea kila tutakapopata nafasi ya kuongelea. 
  Wewe unalipi la kutuambia Kuhusu mtoto wa kiafrika.......................
  
Winnie!


No comments:

Post a Comment